Pages

Monday, February 10, 2014

MOHAMED DEWJI NA JANUARY MAKAMBA WATAJWA KUWA KATI WATU WENYE NGUVU BARANI AFRIKA KWA MWAKA 2014.

Mohammed Dewji mwenye umri wa miaka 39 ametajwa kuwa kati ya watu mashuhuri barani Afrika ambaye anakadiriwa kuwa na utajiri wa dola za kimarekani  $500 kulingana na jarida la forbes africa la hivi karibuni.
Mohammed Dewji
C.E.O of  Mohammed Enterprices (T) LTD

Bwana Dewji ni mwendelezaji wa biashara ya familia yao inayojulikana kwa kama(mohammed enterprises (T) Limited) ambayo ni moja kati ya makampuni makubwa kabisa hapa nchini . Viwanda vya kampuni hii vimeajiri watu takriban 2500 kote nchini na kulingana na mwenyewe Dewji anasema kuwa kampuni hii inaingiza mapato ya dola za kimarekani bil.1.2 kwa mwaka. Vilevile Bw.Dewji amekuwa mbunge wa bunge tukufu la tanzania toka mwaka 2005.


January Makamba pia ni mmoja kati ya watanzania waliotajwa katika jarida la Forbse africa.
Vilevile January ni mmoja kati ya watu waliotjwa kuwa ni moja ya viongozi wadogo wa mwaka 2012 (Young globa Leaders). Kwa sasa januari ni waziri wa mawasiliano , sayansi na teknolojia. January Makamba ni mtoto wa mwanasiasa mashuhuri hapa nchini, Mzee Yusuf
Makamba.

Mr.January Makamba
Waziri wa mawasiliano, sayansi na teknolojia

No comments: